Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kupitia Bia yake Kilimanjaro Premium Lager, leo imezikabidhi mabasi mapyaa ya kisasa aina ya Yutong, kila timu basi moja ambayo yote ghama yake ni sh. milioni 450. Pichani, Makamu Mwenyekiti wa Yanga Clement Sanga (kushoto) na Mwenyekiti wa Simba, Aden Rage wakipongezana baada ya kukabidhiwa mabasi hayo, Makao Makuu ya TBL jijini Dar es Salaam. Katikati yao ni Mkurugenzi Mtendaji wa TBL, Robin Goetzsche. Wengine ni viongozi wa timu hizo na viongozi wa TBL.
Mwanzoni mwa hafla hiyo, ni Katibu Mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Angetile Oseah akijadiliana jambo na waandishi wa habari, Majuto Omari (kushoto) na Efraim Kibonde, makao makuu ya TBL ilala jijini Dar es Salaam.
Mabasi ya kifahari aina ya Yutong yakiwa makao makuu ya TBL kusubiri makabidhiano
Mashabiki wa Simba wakiingia na matarumbeta makao makuu ya TBL kwenye makabidhiano ya mabasi hayo
Mashabiki wa Yanga vilevile nao wakiingia na matarumbeta makao makuu ya TBL kwenye makabidhiano ya mabasi hayo
Kisha wakakutana na kuanza kuserebuka pamoja, lakini wakitupiana maneno, vijembe na tambo kwa nyimbo.
Shabiki wa Simba akimtania mwenzake wa Yanga kwa kumuonyesha tatu bila...
Mwenyekiti wa Simba Aden Rage, akiserebuka na shabiki wa Yanga wakati wa hafla hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Executive Solutions ambayo inasimamia udhamini wa Kilimanjaro Premium Lager kwa Simba na Yangay na Taifa Stars , Aggrey Marealle akizungumza wakati wa hafla hiyo
Meneja wa bia ya Kilimanjaro Premium Lager, George Kavishe akizungumza wakati wa hafla hiyo
Shabiki wa Simba akiwatambia wa Yanga
Shabiki wa Yanga akimtambia Rage aliyeketo meza kuu
Makamu Mwenyekiti wa Yanga Clement Sanga akibadilishana hati na Mkurugenzi Mkuu wa TBL Robin Goetzsche
Mkurigenzi Mtendaji Robin Goetzsche akibadilishana hati na Mwenyekiti wa Simba Aden Rage
Stephen Kilindo wa TBL akizungumza wakati wa hafla hiyo
Rage akikabidhiwa mfano wa ufunguo wa basi na Mkurugenzi Mtendaji wa TBL
Sanga akikabidhiwa mfano wa ufunguo wa gari na Mkurugenzi Mtendaji wa TBL
Viongozi na mashabiki wa timu za Yanga na Simba wakiwa mbele ya mabasi hayo wakati wa makabidhiano
Mtaalam kutoka kampuni ya ASAK Enterprises Edward Mongela akimuonyesha dereva wa Yanga Martin Mtui, jinsi ya ku-opareti baadhi ya vitu kwenye basi walilokabidhiwa Yanga
Dereva wa Simba Mohamed Kigomba ndanbi ya basi jipyaaaa la Simba
Mwenyekiti wa Simba Aden Rage akimshikia mpira Makamu Mwenyekiti wa Yanga Clement Sanga wakati akitia sainbi yake kwenye mpira. Katikati ni Mkurugenzi Mtendaji wa TBL. Robin Goetzsche
Bosi katika TBL akipeperusha bendera kuruhusu mabasi yaanze kuondoka Makao makuu ya TBL ambapo yalitembezwa kupitia mitaa mbalimbali na kwenye baadhi ya matawi ya Yanga na ya Simba na kisha kupelekwa makao makuu ya timu hizo. (Picha zote na Bashir Nkoromo)
Home »
» KILIMANJARO PREMIUM LAGER YAZIPA SIMBA NA YANGA MABASI YA KIFAHARI
0 comments:
Speak up your mind
Tell us what you're thinking... !