...

...

TANGAZA BIDHAA AU HUDUMA ZAKO BORA HAPA KWA BEI NAFUU KABISA: SIMU: +255 712 498008, +255 756 646131, EMAIL:nkoromo@gmail.com

TANGAZA BIDHAA AU HUDUMA ZAKO BORA HAPA KWA BEI NAFUU KABISA: SIMU: +255 712 498008, +255 756 646131, EMAIL:nkoromo@gmail.com

...

Blogroll

Thursday, May 16, 2013

ZAIDI YA POLISI 300 KUMWAGWA UWANJA WA TAIFA KATIKA MECHI YA SIMBA NA YANGA

Akizungumza jioni hii katika kipindi cha Spoti Leo cha Radio One, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Afande Kova amesema, mongoni mwa polisi hao watakuwa makachero  watakaokuwa wanafuatilia nyendo za watu watakaojaribu kuvuruga usalama au mwenendo wote wa mpambanao huo utakaopigwa Jumamosi hii.

Yanya na Simba zinakutana Jumamosi zikiwa zimekamiana sana lakini kila timu na sababu zake. Wakati Yanga ambayo tayari imeshatwaa ubingwa ya Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara, bila shaka itajitahidi kuhakikisha inaifunga simba ili kuonogesha ubingwa wake.

Wakati Yanga ikiwa katika mazinmgira hayo, Simba nayo lazima iifunge Yanga ili kuweka heshima japo ilimekwishavuliwa ubingwa.


LINA NA BARNABA KUTUPIWA VILAGO THT? KISA SHOO YA LADY JAY DEE.

LADY JAY DEE

DAR ES SALAAM, Tanzania
Wakati shoo maalumu ya Miaka 13, ya mwanamuziki nguli wa bongo fleva nchini na kiongozi wa bendi yenye msisimko mkubwa ya ‘Machozi Band’, Judith Wambura ‘Lady Jay Dee’ au Jide’ ikizidi kunukia, huenda kwa upande wa wasanii wa Nyumba ya Vipaji ya THT, Linah Sanga na Barnaba  mwaka huu ukawa mchungu kwao kufuatia kuwepo taarifa za kutimuliwa na uongozi wa juu.

Vyanzo kutoka kwa mtu wa karibu wa Linah vimeeleza kuwa mpaka sasa msanii huyo hana raha na wala hajui ataanza vipi katika harakati zake za kimuziki hasa kufuatia hivi karibuni kukacha shoo ya nguli Lady Jay Dee kwa shinikizo kutoka kwa wakubwa zake wa kazi.

Inadaiwa uongozi wa juu wa Linah umekaa kikao na hatua iliyofuatia kwenye kikao hicho ni kuwaondoa kabisa THT na Barnaba kwa tuhuma kwamba huenda wakatia doa wasanii wenzao ndani ya kundi hilo.

“Juzi Lina, haikuwa kawaida yake maana hata alipopigiwa simu na mtu mmoja kwa ajili ya hatua zingine alionekana kuw na hofu, na wala hakutaka kusikia ushahuri wangu ambao nilikuwa nikimhusia kuwa aachane na mawazo hayo kwani jambo analoliwaza huenda likaisha na hata maamuzi yatakayotoka yatakuwa ni kawaida” kilieleza chanzo kutoka kwa mtu wakaribu wa Lina, amabaye hata hivyo alisema kuwa huenda ukweli wa jambo ukawa hadharani.

Taarifa za ndani za uongozi wa THT zilibainisha kuwa mpango wao wa kuwashughulikia wasanii hao upo pale pale na taratibu zinafuata ili zisilete madhara kwa wasanii waliopo ndani ya THT  na watu wa karibu wanaoiunga mkono THT.

“Wewe nani kakwambia kama tumewaadhibu Lina na Barnaba?, ndio kwanza tunakusikia wewe hizo taarifa,  sisi tunafanya mambo yetu wao waache wafanye yao tukiwa nao sie na tunaouwezo wa kuwatimua ili kulinda hadhi ya THT” Kilieleza chanzo hicho ambacho hata hivyo kutokana na usalama wa jina lake tumelihifadhi.

Aidha, katika ‘ku-balance’ uhondo kamili wa habari hizi wasanii hao wote walipotafutwa kwenye simu zao za mkononi hawakuweza kuwa hewani kwa muda mrefu.. na hata alipopigiwa mtu wao mmoja wa karibu naye alizima simu.

Katika kile kinachoeleza kupamba moto shoo hiyo ya Jide, na kujaa kwa taarifa mbalimbali juu ya wasanii watakaopamba shoo ya miaka 13, Mei 31 ndani ya Nyumbani Lounge, Tayari tiketi zimeanza kuuzwa maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Saalam.

Inaelezwa kwamba katika shoo hiyo ya kijanja ndani ya Nyumbani Lounge, patakuwa hapatoshi pale wadau wa burudani na wastaarabu wote watakapojumuika kwa pamoja ku-shoo love kwa Lady Jay Dee  na Machozi Band, huku listi ya mastaa mbalimbali wanatarajia kuhudhuria sambamba na ‘surprise’ kutoka kwa mastaa hao ambao kwa sasa wengi wapo kimya wakihofia kutengwa na wazee wa ‘fitina bin Logiki’.

Awali kulikuwapo na taarifa za kuwapo kwa msanii Matonya, ambaye mtandao wa Lady Jay Dee ulitoa hadharani kuwa mwanamuziki huyo ameshachukua ‘advance’ ingawa inaelezwa kwamba naye ameshamtishwaili ajitoe, lakini akiwa ameshatafuna pesa ya watu.

Mtandao huo wa Jide umenukuu kila kitu juu ya Makubaliano baina ya Capt.Gadna G Habashi na Matonya ambapo pia unaweza kuyasoma kupitia (Ladyjaydee.blogspot.com) Pia ulitoa kwa mara ya kwanza picha,maelezo muhimu na video ya wanamuziki hao wawili Linah na Barnaba wakiingia mkataba wa shoo hiyo na pia kuhamasisha watu kufika Mei 13.

Thursday, May 9, 2013

SIMBA SPORTS CLUB YAANDAA MPANGO MKAKATI (STRATEGIC PLAN)


Simba Sports Club inapenda kuwataarifu wanachama na mashabiki wake kwamba imeingia makubaliano na Open University Consultancy Bureau (Hapa itafahamika kama “OCB”) kwa ajili ya kuandaa mpango mkakati wa klabu (Strategic Plan).

Mchakato huo unaanza mara moja na OCB wameshaandaa timu yao inayoongozwa na Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania (OUT) Prof. Tolly Mbwette ambapo ili kufanikisha hilo imebidi kuunda kamati ya marejeo ya Simba SC (Referral committee) ambayo kazi yake kubwa itakuwa ni kuiongoza OCB :-

Kuhusu makundi/watu/maeneo yatakayotumiwa kufanya utafiti.

Kunyambulisha kitaalamu nguvu, mianya na maeneo ya maboresho ya mfumo mzima wa Simba SC (SWOT analysis)

Kupitia mpango mkakati ukishaandaliwa baada ya kukusanya maoni ya wanachama, wadau na mashabiki wa klabu kabla ya kuupeleka katika kamati ya utendaji kwa kupitishwa ili ukapitishwe na mkutano mkuu wa wanachama.

Katika kikao cha kamati ya Utendaji ya Simba Sports Club kilichofanyika tarehe 8/5/2013   Referal Committee ya Simba Sports Club iliyochaguliwa ni:- Joseph Itang’are, Swedy Mkwabi
Francis Waya, Ramesh Patel, Evance Aveva, Mulamu Ng’hambi, Salim Mhene, Mtemi Ramadhani
Moses Basena, Henry Tandau, Omary Gumbo, Michael Wambura, Glory Ngahyoma
Crensencius Magori, Honest Njau, Ruge Mutahaba, Evodius Mtawala, Dr Mwafyenga

Kikao cha kwanza kati ya OCB na Kamati husika kitakuwa siku ya tarehe 25/5/2013.

Uongozi wa Simba Sports Club unawataarifu wanachama na wadau kwamba, mpango mkakati huu ndio mwanzo wa mabadiliko ya klabu kuelekea katika kujiendesha kiweledi (professionalism) kwani utabainisha malengo ya klabu kwa kipindi maalumu yakiwemo masuala muhimu kama ujenzi wa uwanja, academy set up, miundo mbinu ya klabu, masuala ya biashara za klabu yakilenga kukuza taswira (brand) ili kufanikisha mauzo ya bidhaa zenye nembo ya klabu, malengo ya mafanikio ya ndani ya uwanja, kujiwekea kiwango/kipimo cha utendaji wa klabu na wanachama (brand goodwill) ili kuvutia wawekezaji.

Mpango mkakati huo pamoja na hayo pia utaweka mipango hiyo katika uhalisia wa utekelezaji na muda wa kutekeleza masuala hayo, jambo litakalofanikisha kuleta kipimo cha utendaji wa uongozi na watendaji wa klabu katika uwajibikaji kwa wadau na wanachama wa klabu.

Mpango mkakati huo utakuwa tayari kwa ajili ya kuingizwa katika mkutano mkuu wa klabu wa mwaka 2013/2014.


Imetolewa na

Evodius Mtawala
Katibu Mkuu,
Simba Sports Club.
9/5/2013

SEMINA YA KUJADILI CHANGAMOTO ZA SOKO LA MUZIKI AFRIKA MASHARIKI 'DOADOA' YAFANYIKA UGANDA

Waendesha mada katika semina ya kuangalia changamoto katika soko la muziki Afrika Mashariki na njia za kuzitatua wakijadili umuhimu wa elimu ya muziki katika soko la muziki, kutoka kulia ni Katibu Mtendaji wa Action Music Tanzania, Mandoli Kahindi, Mkurugenzi wa sanaa kutoka Global Music Academy Ujerumani,William Ramsay, Muaandaaji wa muziki wa Uganda, Kazi Kasozi na Mkurugenzi Mtendaji wa Ketebul Music Kenya, Tabu Osusa

Semina hiyo ambayo inaambatana na maonyesho ya kazi mbalimbali za muziki yameandaliwa na Bayimba Cultural Foundation ya Uganda ambapo wadau mbalimbali wa muziki kutoka nchi mbalimbali wamejumuika kujadili na kubadilishana uzeofu juu ya soko la muziki kwa nchi za Afrika Mashariki. picha za matukio zaidi tembelea DOADOA

Thursday, May 2, 2013

TBL YAHIMIZA POOL KUENEZWA MIKOA YOTE TANZANIA BARA


VYAMA vya mchezo wa pool kuanzia wilaya hadi taifa vimetakiwa kutumia vizuri udhamini wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) kuhakikisha mchezo huo unaenea katika mikoa yote ya Tanzania Bara.

Hayo yalisemwa jana na diwani wa kata ya Kitanzini katika Manispaa ya Iringa, Jesca Msambatavangu wakati alipokuwa mgeni rasmi wakati wa kukabidhi vifaa vya michezo kwa vyuo vikuu vitakavyoshiriki mashindano ya mchezo huo kwa wanafunzi wa elimu ya juu ngazi ya mkoa wa Iringa ya 'Higher Learning Pool Competition 2013'.

Msambatavangu alisema kuwa ni vema vyama vya mchezo huo vikatumia nafasi ya udhamini huo vizuri katika kuhakikisha mchezo wa pool unapanuka zaidi ili hatimaye uchezwe kila mkoa kwa mikoa yote ya Tanzania Bara kuanzia kwenye klabu na vyuo vikuu.

"Nitakuwa mchoyo wa fadhila kama sitawashukuru na kuwapongeza TBL kupitia bia ya Safari Lager kwa kuutoa mbali mchezo wa pool na hatimaye kuufikisha hapa ulipo na pia udhamini wa kampuni yenu si katika mchezo wa pool pekee bali ni mambo mengi mnayoyafanya kwenye jamii katika kuchangia maendeleo ya taifa letu na serikali inalitambua hilo,"alisema Msambatavangu.

Aliongeza kwa kuwataka vijana wengi kuendelea kujitokeza kujifunza kucheza mchezo huo ambao kwa sasa ni ajira kwa vijana wanaoucheza.

Katika kile kilichoonekana kuwa ni mmoja wa wadau wa mchezo huo, diwani huyo aliahidi kutoa mbuzi mmoja mmoja kwa kila chuo kinachoshiriki mashindano hayo.

Naye mwenyekiti wa chama cha mchezo huo mkoa wa Iringa (IRPA), Salim Kisaku alisema kuwa mashindano hayo yatakayoshirikisha vyuo vikuu vinne yatafanyika kesho kwenye ukumbi wa Twisters Club.

Kisaku alivitaja vyuo vitakavyoshiriki mashindano hayo kuwa ni Ruaha, CDTI, Mkwawa na Tumaini.
Alisema kuwa chuo kitakachobeba ubingwa wa mkoa huo ndiyo kitakachoushirikisha katika fainali za taifa za mashindano hayo zitakazofanyika juni mosi jijini Dar es Salaam.

Meneja wa Kampuni ya TBL mkoani hapa, Josephat Changwe alisema kuwa bingwa wa mashindano hayo kwa upande wa timu katika mkoa huo atajinyakulia fedha taslim Sh.500,000, mshindi wa pili Sh.300,000, mshindi wa tatu Sh.200,000 na mshindi wa nne Sh.100,000.

Changwe alisema kuwa kwa upande wa mchezaji mmoja mmoja (wanaume) bingwa atazawadiwa Sh.150,000 na mshindi wa pili Sh.100,000 wakati kwa upande wa wanawake bingwa atapewa Sh.100,000 na mshindi wa pili Sh.50,000.

Meneja wa Kampuni ya Bia Tanzania(TBL) Mkoa wa Iringa, Josephat Changwe (kushoto) akimkabidhi tisheti Diwani wa Kata ya Kitanzini Manispaa ya Iringa Mjini, Jesca Msambatavangu ili awakabidhi vyuo shirika vya elimu ya juu kwenye mashindano ya Pool kwa vyuo hivyo Iringa jana.Kulia ni Mwenyekiti wa chama cha Pool Mkoa wa Iringa Salum Kisaku.
4
Diwani wa Kata ya Kitanzini Manispaa ya Iringa Mjini, Jesca Msambatavangu(wa pili kushoto) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa hafla fupi ya kukabidhi vifaa vya michezo kwa vyo shiriki vya mashindano ya Pool yanayotarajiwa kuanza kesho Mkoa wa Iringa.Kushoto ni Meneja wa Kampuni ya Bia Tanzania(TBL) Mkoa wa Iringa, Josephat Changwe.Kutoka kulia ni Katibu wa chama cha pool Mkoa wa Iringa,Haji Kiyeyeu na Mwenyekiti wa chama hicho,Salum Kisaku.
1.JPGDiwani wa Kata ya Kitanzini Manispaa ya Iringa Mjini, Jesca Msambatavangu (kushoto) akimkabidhi tisheti nahodha wa timu ya chuo Kikuu cha Ruaha, Said Mohamed wakati wa hafla fupi ya kukabidhi vifaa vya michezo kwa vyuo shiriki vya mashindano ya Pool kwa Vyuo vya Elimu ya Juu Mkoa wa Iringa.Katikati Kushoto ni Mwenyekiti wa Chama cha Pool Mkoa wa Iringa,Salumu Kisaku na Katibu wa chama hicho,Haji Kiyeyeu.
View   Share   Download  

CHEKA AENDELEZA UBABE NCHINI AMDUNDA THOMAS MASHALI KWA 'KO'

Bondia Fransic Cheka Kushoto akipambani na Thomas Mshali wakati wa mpambano wao uliofanyika katika sikukuu ya mei mosi katika ukumbi wa PTA Sabasaba Dar es salaam Cheka alishinda kwa KNOCKOUT raundi ya kumi. 
Bondia Fransic Cheka Kushoto akimshambilia kwa makonde ya nguvu Thomas Mshali wakati wa mpambano wao uliofanyika katika sikukuu ya mei mosi katika ukumbi wa PTA Sabasaba Dar es salaam Cheka alishinda kwa KNOCKOUT raundi ya kumi
Bondia Shabani Mhamila 'Star Boy' kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana masumbwi na Yusuph Jibaba wakati wa mpambano wao uliofanyika mei mosi katika ukumbi wa PTA Saba saba Dar es salaam Star Boy alishinda kwa KNOCKOUT raundi ya nne
Bondia Shabani Mhamila 'Star Boy' kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana masumbwi na Yusuph Jibaba wakati wa mpambano wao uliofanyika mei mosi katika ukumbi wa PTA Saba saba Dar es salaam Star Boy alishinda kwa KNOCKOUT raundi ya nne
Bondia Shabani Mhamila 'Star Boy' kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana masumbwi na Yusuph Jibaba wakati wa mpambano wao uliofanyika mei mosi katika ukumbi wa PTA Saba saba Dar es salaam Star Boy alishinda kwa KNOCKOUTraundi ya nne
Bondia Shabani Mhamila 'Star Boy' akishangilia ushindi uku akiwa amebebwa juu juu kama mkungu wa ndizi.
Bondia Cosmas Cheka kushoto akipambana na Charles Mashali wakati wa mpambano wao uliofanyika katika ukumbi wa PTA Sabasaba siku ya mei mosi Cheka alishinda kwa ponti mpambano huo
Kocha wa Kimataifa wa Mchezo wa Masumbwi Rajabu Mhamila 'Super D' akimsindikiza wakati wa kupigana bondia Ibrahimu Class 'King class Mawe wakati wa mpambano wake na amos mwamakula
Bondia Amos Mwamakula kushoto na Ibrahimu Class 'King Class mawe' wakisubili matokeo ambapo class alishinda kwa point
Bondia Thomas Mashali kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Fransic Cheka katika ukumbi wa PTA Sabasaba Dar es salaam Cheka alishinda kwa KNOCKOUT
Shomari kimbau akiwa na Cheka baada ya kumvisha ubingwa wa IBF Africa aliokuwa akiutetea
Kotoka kushoto ni Kocha wa mchezo wa ngumi Kimataifa Rajabu Mhamila 'Super D' mdau ambaye ajajulikana jina Mtaalishaji wa mpambano kati ya Fransic Cheka Vs Thomasi Mashali Adamu Tanaka 'Tunaluza' na MC wa mpambano huo COOL p
Rashidi Mhamila 'Ngade akiwa amepozi na Bady Boy wakati wa onesho hilo. Picha zote na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Tuesday, April 30, 2013

JAHAZI MODERN TAARAB KUUPAMBA MKESHA WA MEI MOSI NDANI YA DAR LIVE LEO